Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba, 2025

SERIKALI YAAHIDI ULINZI NA USHIRIKIANO KWA WAANDISHI WA MITANDAONI

Picha
Dar es Salaam - Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuonesha dhamira ya dhati ya kulea na kuwawezesha waandishi wa habari wa mitandaoni na mabloga, badala ya kuwashughulikia kwa mtazamo wa adhabu, ili kujenga tasnia imara na yenye tija ya habari nchini. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa, aliipongeza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa mwelekeo wake wa kulea wadau wa sekta ya habari badala ya kuchukua hatua kali za kinidhamu. Msigwa alisema mwelekeo huo unaendana na falsafa ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambayo inalenga kushirikiana na wadau mbalimbali kwa manufaa ya taifa. Aliitaja Tanzania Bloggers Network (TBN) na Jukwaa la Mitandao Tanzania (JUMIKITA) kuwa ni wadau wakubwa wa serikali katika tasnia ya habari, akisisitiza kuwa mchango wao ni muhimu katika kusambaza taarifa na kujenga mawasiliano kati y...

MEYA WA JIJI LA ARUSHA AELEZA MAFANIKIO YA ZIARA YA WAZIRI WA TAMISEMI KATIKA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO.

Picha
Meya wa Jiji la Arusha, Mheshimiwa Maximilian Iranque, amezungumzia kwa kina ziara ya kikazi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe, iliyofanyika jijini Arusha kwa lengo la kukagua na kutathmini utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Jiji hilo. Katika ziara hiyo, Profesa Shemdoe alitembelea na kukagua miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo ujenzi wa Soko la Kilombero, uwanja wa mpira, pamoja na jengo la Utawala la Jiji la Arusha. Waziri alipata fursa ya kujionea hatua kubwa zilizofikiwa katika utekelezaji wa miradi hiyo, ambayo inalenga kuboresha huduma kwa wananchi na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika jiji. Akizungumza baada ya ziara hiyo, Meya Iranque amesema kuwa Waziri wa TAMISEMI ameridhishwa na kasi, ubora pamoja na usimamizi wa miradi hiyo, akisisitiza kuwa miradi hiyo ina mchango mkubwa katika kuinua uchumi wa Jiji la Arusha, kuongeza fursa za ajira kwa wananchi, pamoja na kuboresha mazingira ya biashara na utoaji wa huduma za kij...

RC MAKALLA AWATAKA MADIWANI JIJI LA ARUSHA KUSIMAMIA MIRADI NA UTATUZI KERO ZA WANANCHI

Picha
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla ameliagiza Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Arusha kusimamia vyema makusanyo ya mapato, kuboresha utoaji wa huduma katika Vyanzo hivyo akisitiza kuwa mapato ndio msingi wa Halmashauri katika ujenzi wa uwezo wa kuhudumia jamii. Mhe. Makalla ameagiza hayo leo Jumanne Disemba 16, 2025 wakati wa Kikao cha Baraza la Madiwani Jiji la Arusha, akiwataka pia kutimiza majukumu yao kwa umoja na ushirikiano pamoja na kuwatumia Vyema wataalamu wa Halmashauri hiyo katika utekelezaji wa majukumu yao. "Mapato ni msingi wa Halmashauri katika kuwahudumia wananchi wenu. Wekeni mikakati katika kukusanya, kuvisimamia vyanzo vya mapato na kuboresha huduma kwenye vyanzo vyenu vya mapato ikiwemo masoko. Takwimu za ukusanyaji mapato bado haziridhishi." Amesema CPA Makalla. Mhe. Makalla pia amewataka Madiwani hao kuwa na usimamizi mzuri wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye maeneo yao, akitaka miradi yote ikamilike kwa wakati kuli...

RC MAKALLA AWAPONGEZA WANANCHI KWA KUYAKATAA MAANDAMANO YA DISEMBA 09

Picha
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla leo Jumatano Disemba 10, 2025, amewapongeza wananchi kwa kuyakataa maandamano ya Disemba 09, 2025, akiwataka kujenga utamaduni wa kudumu wa kukataa maandamano na matukio yote yenye viashiria vya uvunjifu wa amani Mkoani Arusha. Mhe. Makalla amebainisha hayo wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za kibiashara kwenye soko la Kilombero Jijini Arusha, akiahidi kuwa serikali na Vyombo vya ulinzi na usalama Mkoani Arusha vitaendelea kuhakikisha usalama na amani inakuwepo. "Dunia imeona na watanzania wameithibitishia dunia ya kwamba wakiamua kulinda amani wanailinda, wasiotutakia mema jana wameaibika. Watanzania wanapenda amani na hawajazoea mambo ya maandamano na uvunjifu wa amani na wale wote waliokuwa wanataka vurugu leo wamejifungua- wana maumivu kwani hawakufanikiwa." Amesema Mhe. Makalla. Mhe. Makalla kadhalika kando ya kuwahakikishia wananchi ulinzi na usalama muda wote, amehimiza pia umuhimu wa wananchi kujikita katika...

RC MAKALLA AWAHAKIKISHIA USALAMA WANANCHI WA ARUSHA

Picha
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla amewahakikishia usalama na utulivu wananchi wa Mkoa wa Arusha, akiwataka kuendelea na shughuli zao na kusema Vyombo vya ulinzi na usalama vipo tayari muda wote kuwalinda wao na mali zao. Mhe. Makalla amebainisha hayo leo Jumatatu Disemba 08, 2025, wakati akizungumza na wananchi wanaoishi kwenye Mpaka wa Namanga, Wilayani Longido, unaounganisha Tanzania na Kenya, mara baada ya Kikao cha ujirani mwema cha Kamati za usalama za Mikoa ya Arusha na Rift Valley ya nchini Kenya. "Nipo hapa kuwahakikishia Serikali na Vyombo vyote vya ulinzi na usalama vipo tayari kuwalinda Watanzania na mali zao zote na kwa maana hiyo kesho wana Arusha endeleeni na kazi zenu kama kawaida. Ni mapumziko lakini kazi za kiuchumi ziendelee kama kawaida kwani marufuku iliyopigwa ni ya maandamano." Amesema Mhe. Makalla Akisisitiza wajibu wa serikali katika kulinda raia na mali zao, Mhe. Makalla pia amewahimiza Wananchi wanaoishi kwenye eneo hilo la mpaka k...

TANZANIA NA MAREKANI ZASONGA MBELE KUKAMILISHA MAKUBALIANO MAKUBWA YA UWEKEZAJI

Picha
  Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo amefanya mazungumzo na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Andrew Lentz, katika Ikulu ya Chamwino, kujadili maeneo muhimu ya ushirikiano na kuimarisha dhamira ya pamoja ya kujenga ushirikiano wa kisasa na wenye manufaa kwa pande zote mbili. Balozi Lentz—aliyefuatana na Mshauri wa Masuala ya Kisiasa na Uchumi—amesisitiza dhamira ya Washington kuhuisha mahusiano na kuongeza kina la ushirikiano wa kiuchumi, kisiasa na kiusalama kati ya mataifa haya mawili. “Marekani imejitolea kujenga ushirikiano usiotegemea misaada, bali unaojengwa juu ya ustawi wa pamoja,” alisema Balozi Lentz. Mazungumzo yamejikita katika hatua za majadiliano ya miradi mikubwa inayoongozwa na kampuni za Marekani. Pande zote mbili zimekubaliana kuwa majadiliano ya miradi miwili ya kimkakati—Mradi wa LNG na Mradi wa Tembo Nickel—yamefikia hatua za mwisho kabla ya kutiwa saini rasmi. Uwekezaji wa tatu, Mradi wa Mahenge Graphite, ...

TANZANIA AND U.S. MOVE TO FINALISE MAJOR INVESTMENT AGREEMENTS

Picha
Her Excellency Dr. Samia Suluhu Hassan, President of the United Republic of Tanzania, today held talks with the Acting United States Ambassador to Tanzania, Andrew Lentz, at Chamwino State House to advance key areas of bilateral cooperation and reaffirm the shared commitment to a modern, mutually beneficial partnership. Ambassador Lentz—accompanied by the Counselor for Political and Economic Affairs—underscored Washington’s determination to reset the relationship and deepen economic, political, and security collaboration with Tanzania. “The United States is committed to a partnership based not on aid dependency but on shared prosperity,” Ambassador Lentz said. The discussions centred on ongoing negotiations involving major U.S.-linked strategic investments. Both sides acknowledged that talks on two flagship projects—the LNG Project and Tembo Nickel Project—are now in their final stages, pending formal signing. A third investment, the Mahenge Graphite Project, remains under active techn...

*KENYA YAWAKATAA WACHOCHEZI WA MAANDAMANO YA TANZANIA*

Picha
*_Waahidi Ushirikiano wa kulinda amani na Mipaka_*   *_Rc Makalla awahakikishia usalama wananchi wa Mpakani_*  Mkuu wa Wilaya ya Oloililai, Rift Valley nchini Kenya Mhe. Andrew Mwiti Mathew amesema serikali ya Kenya haiungi Mkono wachochezi wa vurugu, ghasia na maandamano nchini Tanzania, akiahidi kuzuia Wakenya kuchochea na kushiriki kwenye vurugu na maandamano haramu. Mhe. Mwiti amebainisha hayo leo Disemba 08, 2025 mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla, wakati wa Kikao cha ujirani mwema kilichofanyika Wilayani Longido, ikihusisha Kamati za Ulinzi za Mkoa wa Rift Valley na Mkoa wa Arusha, kama sehemu ya kuimarisha usalama na biashara kwenye eneo la mpaka wa Namanga. "Sisi tuwahakikishie kuwa tumejipanga vizuri kuzuia wachochezi na mtu yeyote ambaye anaweza kuwa na nia ya kuja kujiunga na wale watakaokuwa wanapanga kufanya maandamano ambayo tayari tumehakikishiwa kuwa ni haramu kwani hayajaruhusiwa kisheria." Amesisitiza Mhe. Mwiti. Awali katika m...

BARAZA JIPYA LA ARUSHA LATOA AHADI KUBWA

Picha
  Baraza jipya la madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Arusha limeanza rasmi majukumu yake baada ya madiwani 34 kuapishwa, likiahidi kuleta mabadiliko yenye tija kwa wananchi na kusimamia kwa nguvu mapambano dhidi ya rushwa. Katibu Tawala wa Wilaya ya Arusha Mjini, Jacob Rombo, amesisitiza kuwa madiwani wanapaswa kutekeleza kazi zao kwa kuzingatia misingi ya utawala bora na kuepuka kuingilia majukumu ya wataalamu wa halmashauri, hasa kwenye eneo la mipango miji. Amewataka viongozi hao kuishi viapo vyao na kuhakikisha wanawawekea wananchi mazingira ya kupata maendeleo ya kweli. Naibu Meya wa Jiji la Arusha, Julius Medeye, ameahidi umoja na mshikamano ndani ya baraza, akiongeza kuwa jukumu lao kubwa ni kuwatumikia wananchi pasipo makundi wala mgawanyiko. Amewataka madiwani kushughulikia kwa bidii changamoto za kata zao, hususan upatikanaji wa huduma za maji, barabara na miundombinu mingine muhimu. Meya wa Jiji, Maxmillian Irangne, amesema kuwa baraza litaendeleza miradi iliyoanzishwa i...

WANAOBEZA KAULI YA MSIGWA HAWAFAHAMU UWAJIBIKAJI WA VYOMBO VYA HABARI WAKATI WA MACHAFUKO.

Picha
Pongezi za Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, kwa waandishi wa habari nchini kutokana na namna walivyotekeleza wajibu wao wakati wa vurugu za Oktoba 29, zimezua mijadala mikubwa katika mitandao ya kijamii. Wapo waliozipokea kwa mtazamo chanya na wapo wanaozihoji au kuzibeza. Hata hivyo, uchambuzi wa kina unaonesha kwamba wanaozishambulia pongezi hizo mara nyingi hawatambui uzito, hatari, na dhamana kubwa ya vyombo vya habari wakati wa matukio ya sintofahamu. Kwa hakika, katika nyakati za misukosuko, waandishi hawabebi kalamu tu hubeba ustawi wa taifa, amani ya jamii, na mara nyingi hutengeneza mazingira ya kuokoa nchi dhidi ya jazba. Akizungumza kuhusu kauli ya Msigwa, mwandishi mkongwe na Mwenyekiti wa Tanzania Bloggers Network (TBN), Beda Msimbe, alitoa mtazamo wa kitaalamu juu ya umuhimu wa pongezi hizo.  “ Waandishi waliokoa Amani Katika mazingira ya kawaida kabisa, Msemaji Mkuu alifanya vyema kutoa pongezi. Waandishi walionesha ukomavu, uzalendo na uwajibikaji mkubwa. W...

TBN YATOA UFAFANUZI KUHUSU MKUTANO WA IKULU

Picha
DAR ES SALAAM MTANDAO wa Wanablogu Tanzania (TBN) unapenda kutoa ufafanuzi rasmi na kuweka mambo wazi kufuatia taarifa zisizo sahihi na zinazoleta utata zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu mkutano uliofanyika hivi karibuni Ikulu. TBN inakanusha vikali madai yanayosambazwa na baadhi ya watu wanaojiita wanaharakati, wakidai—bila uthibitisho wowote—kuwa wanahabari wa maudhui ya mtandaoni waliitwa Ikulu jijini Dar es Salaam kwa lengo la "kupewa maelekezo" kuhusu maandamano yanayodaiwa kupangwa kufanyika tarehe 9 Desemba. Kusudi Halisi la Mkutano TBN inathibitisha kuwa madai haya si sahihi na yamekuwa yakipotoshwa. Kusudi la kweli na la moja kwa moja la wito wa Ikulu lilikuwa hili: Mkurugenzi mpya wa Mawasiliano Ikulu, Bw. Bakari Machumu, alifanya mkutano wa utambulisho rasmi na wadau muhimu wa sekta ya habari, akianza na wanahabari wa maudhui ya mtandaoni. Mkutano huu ulikuwa ni hatua muhimu ya kuweka msingi wa ushirikiano na mawasiliano bora. Hakukuwa na ajenda iliy...

VERONICA MREMA KWA KUCHAGULIWA KUHUDHURIA MKUTANO WA KIMATAIFA WA WAANDISHI WA HABARI ZA KISAYANSI!

Picha
Kilele cha utambuzi wa uandishi wa habari za kidijitali nchini Tanzania kimethibitishwa baada ya Bi. Veronica Mrema, Mwanzilishi wa chombo cha habari cha M24 TANZANIA MEDIA na mwanachama mahiri wa Tanzania Bloggers Network (TBN), kuingia rasmi kwenye jopo la mdahalo katika Mkutano wa 13 wa Kimataifa wa Waandishi wa Habari za Sayansi (WCSJ2025) unaofanyika jijini Pretoria.  Hili si tu fahari kwa Mrema binafsi, bali ni heshima kubwa kwa TBN na tasnia nzima ya habari nchini, ikionesha kuwa kazi ya uandishi wa kidijitali inatambulika katika majukwaa makuu duniani. Mrema yuko Afrika Kusini kuhudhuria mkutano huo mkuu unaotarajiwa kudumu hadi Desemba 5, 2025, baada ya kukabidhiwa udhamini maalum wa safari (Travel Grant) na Wizara ya Sayansi, Teknolojia, na Ubunifu ya Afrika Kusini (DSTI).  Udhamini huu ulikuja kama matunda ya utambuzi wa utendaji wake wa kipekee katika uandishi wa habari za kisayansi na afya, akibainishwa kuwa miongoni mwa wachache barani Afrika waliochaguliwa kwa h...