Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2025

MSIMAMIZI WA UCHAGUZI ARUSHA MJINI: WALIOPOTEZA KADI YA KURA WATARUHUSIWA KUTUMIA NIDA, LESENI AU PASI YA KUSAFIRI.

Picha
Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Arusha Mjini ametangaza rasmi kuwa Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani utafanyika siku ya Jumatano, tarehe 29 Oktoba 2025, kwa mujibu wa Kifungu cha 69(1) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya mwaka 2024. Kwa mujibu wa tangazo hilo, vituo vilivyotumika kuandikisha wapiga kura ndivyo vitakavyotumika kupigia kura siku ya uchaguzi. Vituo hivyo vitafunguliwa saa 1:00 asubuhi (2:00) na kufungwa saa 10:00 jioni (10:00). Aidha, kwa wapiga kura wa magereza, vituo vyao vitafunguliwa saa 2:00 asubuhi (2:00) na kufungwa saa 9:00 alasiri (9:00). Taarifa Muhimu kwa Wananchi Sambamba na tangazo hilo, kwa kila kituo cha kupigia kura zimebandikwa taarifa zifuatazo: Mfano wa karatasi ya kura yenye majina, picha, na nembo za vyama vya wagombea wa nafasi za Rais, Wabunge na Madiwani; Orodha ya majina ya wapiga kura walioandikishwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi; Orodha ya wapiga kura waliopangiwa kupiga kura ya Rais pekee. Wananchi wote wanahi...

(DCEA) ΤΑΝΙ ΤΑΝΟ YA BANGI YA ARUSHA YACHOMWA MOTO, WANANCHI WATAKA MAZAO MBADALA IKISHINDIKANA TUTATUMIA NGUVU

Picha
MAMLAKA YA KUDHIBITI NA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA (DCEA) KANDA YA KASKAZINI KWA NIABA YA KAMISHNA JENERALI ARETAS LYIMO TAREHE 09.10.2025 KWA MUJIBU WA SHERIA IMETEKETEZA DAWA ZA KULEVYA AINA YA BANGI (KAVU) JUMLA YA TANI TANO NA KILOGRAMU 200 KATIKA ENEO LA MAKAO MAPYA YALIYOPO KIJIJI/KATA YA UWIRO  WILAYANI ARUMERU KATIKA MKOA WA ARUSHA. UTEKETEZAJI HUU UMEFANYANYIKA KWA AMRI YA MAHAKAMA AMBAPO TAASISI ZOTE ZA SERIKALI ZINAZOTAJWA KISHERIA KATIKA UTEKETEZAJI WA VIELELEZO VYA DAWA ZA KULEVYA ZIMESHIRIKI. VIELELEZO HIVI VILIVYOTEKETEZWA NI MATOKEO YA MAFANIKIO YA OPERESHENI YA PAMOJA YA KUDHIBITI UZALISHAJI NA USAFIRISHWAJI WA BANGI WILAYANI ARUMERU ZILIZOFANYIKA HIVI KARIBUNI KWA KUSHIKISHA WANANCHI, SERIKALI YA WILAYA YA ARUMERU NA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUPITIA SHIRIKA LA HIFADHI ZA TAIFA (TANAPA). MAMLAKA INATOA RAI KWA WANANCHI KUTOJIHUSISHA KWA NAMNA YEYOTE NA UHALIFU WA DAWA ZA KULEVYA KWANI ADHABU YAKE NI HADI  KIFUNGO CHA MAISHA JELA. ##MWISHO##

ELIMU YA WATU WAZIMA YAZIDI KUPAA ARUSHA

Picha
Mgeni Rasmi katika hafla ya maadhimisho ya wiki ya Elimu ya Watu Wazima Wilaya ya Arusha,Bi. Chausiku Baha akivalishwa skafu na mmoja wa Wanafunzi waliopata elimu nje ya mfumo rasmi. Mamamia ya wananchi, walimu, wanafunzi na wadau wa elimu wamejitokeza leo kushiriki maadhimisho ya Wiki ya Elimu ya Watu Wazima na Elimu Nje ya Mfumo Rasmi yaliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Levolosi, jijini Arusha. Maadhimisho hayo, yaliyopewa kauli mbiu “Elimu Endelevu kwa Maendeleo ya Jamii”, yamelenga kuhamasisha jamii kuhusu nafasi ya elimu kwa kila Mtanzania bila kujali umri au changamoto zilizomkumba awali. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mjini, Afisa Tarafa wa Levolosi, Chausiku Baha alisema serikali imeweka mikakati ya kuhakikisha wananchi wote wanapata elimu bora na stadi za maisha zitakazowasaidia kuboresha maisha yao. “Elimu ya watu wazima imekuwa kichocheo cha maendeleo ya kijamii na kiuchumi ,tunawahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki programu hiz...