Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2025

DCEA YAHITIMISHA MAFUNZO YA KIMATAIFA KATIKA KUWAJENGEA UWEZO ASASI ZA KIRAIA JIJINI ARUSHA*

Picha
DCEA yazijengea uwezo Asasi za Kiraia Arusha kwa kuwapa miongozo sahihi ya uelimishaji umma ngazi ya familia_* Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Kanda ya Kaskazini kwa kushirikiana na Taasisi ya Colombo Plan Drug Advisory Programme (CP-DAP) tarehe 22.05.2025 imehitimisha mafunzo maalum ya siku 5 ya kuwajengea uwezo Asasi za Kiraia juu ya Mtaala wa Kimataifa wa utoaji elimu kinga sahihi dhidi ya tatizo la dawa za kulevya kwa ngazi ya familia (Universal Prevention Curriculum-UPC Family Based Prevention) kwa Wawakilishi wa Asasi za Kiraia 24 katika Ukumbi wa YCR uliopo Ngarenaro jijini Arusha.  Mafunzo hayo ya siku tano yamewaweza washiriki hao kupata mbinu mpya zilizothibitishwa kisayansi zitakazowasaidia katika kutoa elimu kinga ngazi ya familia.  Aidha, washiriki wa mafunzo hayo walipatiwa vyeti vinavyotambulika kimataifa katika utoaji elimu sahihi dhidi ya tatizo la dawa za kulevya. Hivyo, wataalamu hao wataenda kuisaidia jamii ya kitanzania katika k...

NCAA YANADI VIVUTIO VYA UTALII MAADHIMISHO YA SIKU YA NYUKI DUNIANI YALIYOFANYIKA DODOMA

Picha
Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imetumia fursa ya maadhimisho ya Siku ya Nyuki Duniani yanayofanyika jijini Dodoma kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii  vinavyopatikana katika Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.  Maadhimisho hayo yaliyoanza Mei 17 na kuhitimishwa leo Mei 20, 2025 katika Viwanja vya Chinangali Park Dodoma Mgeni rasmi akiwa ni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa, yamewakutanisha wadau wa sekta ya nyuki kutoka Mikoa mbalimbali nchini kujadili maswala yanayohusu sekta ya ufugaji nyuki katika uhifadhi na kuleta maendeleo endelevu kwa jamii. Katika maadhimisho hayo NCAA imepata fursa ya kutangaza vivutio vyake vya utalii vikiwemo Bonde la kreta ya Ngorongoro lenye muonekano wa pekee, wanyama mbalimbali ikowemo wa wanyama wakubwa watano “The big Five “,  Laitoli zinakopatikana Nyayo za binadamu wa kale aliyeishi miaka milioni 3.7 iliyopita, Olduvai George eneo lenye gunduzi za kihistoria ya akiolojia, Kreta ya Empakai iliyop...

MAGEUZI MAPYA KATIKA SEKTA YA MILIKI YALENGA KUIMARISHA MAKAZI NA BIASHARA

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi iko mbioni kuandaa sera mpya pamoja na kupitia sheria mbalimbali zitakazotambua kada ya Miliki, Wathamini na Madalali nchini. Akizungumza jijini Arusha katika mkutano wa tano wa mwaka wa wadau wa Miliki Kuu, Waziri wa wizara hiyo, Deogratius Ndejembi, amesema kuwa serikali imelenga kuimarisha sekta ya makazi na kupanua wigo wa biashara. Amesema mchango wa wataalamu wa miliki ni mkubwa katika kukuza na kuimarisha miundombinu ya nchi, jambo linalokwenda sambamba na dhamira ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. “Mageuzi haya yanaendana na maboresho ya miundombinu kama Reli ya Kisasa, barabara, usafiri wa anga na maji,” amesema Ndejembi, huku akiahidi ushirikiano wa karibu kati ya serikali na wataalamu wa sekta hiyo. Rais wa Chama cha Wataalamu wa Miliki Kuu nchini, Andrew Kato, amesema kutokuwepo kwa sera maalumu ya makazi kumechangia changamoto nyingi katika sekta hiyo na kuathiri utekel...

WIZI WA BIMA WAFUMULIWA, SERIKALI YA PANGA MASHAMBULIZI

Picha
Serikali imepiga kengele ya tahadhari kufuatia ongezeko la madai feki ya bima yanayodaiwa kuisababishia nchi hasara ya mabilioni, huku ikiweka wazi kuwa asilimia 10 hadi 15 ya madai hayo duniani yana chembechembe za udanganyifu. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Zanzibar, Dk. Sada Mkuya, amesema hali hiyo imeifanya sekta ya bima kupoteza uaminifu wa umma na kuathiri utoaji wa huduma kwa wateja wa kweli wanaohitaji msaada halali. Akizungumza kwa niaba ya Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi, wakati wa mkutano wa wataalamu wa udhibiti wa udanganyifu wa bima (IASIU), Dk. Sada alisema baadhi ya maofisa wa bima wanashirikiana na wateja kudanganya kwa malipo hewa, jambo alilolieleza kuwa ni uhujumu uchumi. “Fedha zinazopotea kwa njia ya hila hizi zingetumika kuboresha huduma kwa wananchi Serikali haiwezi kufumbia macho wizi huu unaotendeka kwa hila ya taaluma,” alisema na kupendekeza kuanzishwa kwa mahakama au kitengo maalum kitakachoshughulikia uhalifu wa bima kwa haraka na kw...