Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2026

MEYA ATOA SAA TATU KONΤΕΝΑ LENYE UCHAFU NA HARUFU KALI YA TAKA KUONDOLEWA,ACHAFUKWA AAHIDI KUMWAJIBISHA.

Picha
MASTAHIKI Meya wa Jiji la Arusha, Maximilian Iranghe, ameweka msimamo mkali dhidi ya uzembe katika usimamizi wa usafi wa mazingira jijini humo, akiahidi kumwajibisha Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, James Lebikoki, kwa kushindwa kusimamia ipasavyo watendaji wake hali iliyosababisha kuendelea kwa kero ya uchafu, hususan katika masoko ya jiji. Akizungumza leo Januari 4, 2026 wakati wa ziara ya kampeni ya "Ng'arisha Jiji" katika Soko la Mitumba Mbauda, kata ya Sombetini, Meya Iranghe alisema suala la usafi si mjadala wa kisiasa bali ni wajibu wa kiutendaji, akionya kuwa hatasita kuchukua hatua kali dhidi ya viongozi na watendaji wanaoshindwa kutimiza majukumu yao. Iranghe alionekana kukerwa na harufu kali na mrundikano wa taka ngumu zilizokuwa zimejaa kwenye kontena la soko hilo, hali ambayo wafanyabiashara walieleza kuwa taka hizo hukaa kwa zaidi ya wiki mbili, kunyeshewa na mvua na kuhatarisha afya zao kutokana na uwezekano wa magonjwa ya mlipuko. Katika hotuba yake, Me...

ARUSHA YAPATA HUDUMA ZA KIBINGWA ZA MOYO, DC MKUDE ASISITIZA KINGA NA UCHUNGUZI WA AFYA WA MARA KWA MARA KWA WANANCHI

Picha
MKUU wa Wilaya ya Arusha, Joseph Mkude, ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Arusha na maeneo ya jirani kuzingatia afya zao kwa kufanya uchunguzi wa mara kwa mara, huku akisisitiza umuhimu wa kujiunga na mpango wa Bima ya Afya kwa Wote kama nguzo muhimu ya kufanikisha azma ya afya bora kwa kila Mtanzania. Akizungumza wakati wa ziara yake katika Kambi Maalum ya Uchunguzi na Matibabu ya Magonjwa ya Moyo inayofanyika katika Hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre (ALMC) Januari 4, 2026, Mkude alisema kuwa magonjwa yasiyoambukiza yameendelea kuwa tishio kubwa kwa afya ya jamii, hususan magonjwa ya moyo, shinikizo la damu na kisukari. Alianza hotuba yake kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema ya uhai, kisha akatoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuimarisha sekta ya afya kupitia programu ya Tiba Mkoba, inayosogeza huduma za kibingwa karibu na wananchi walipo. "Kupitia programu hii, Watanzania wengi wamepata furs...