Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Julai, 2024

BILIONEA MULOKOZI AKABIDHI ZAWADI YA BAJAJI MPYA KWA KIJANA ALIYEWEKA PICHA YAKE KWENYE BAJAJI

Picha
  Bilionea David Mulokozi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Mati Super Brands Limited ametoa zawadi ya Bajaji mpya kwa Dereva wa bajaji Abel Rajabu ambaye ameweka picha ya Bilionea huyo kwenye bajaji yake baada ya kuvutiwa na kazi anazozifanya za kuwekeza kwenye viwanda na kusaidia jamii inayomzunguka kutokana na faida anayoipata. David Mulokozi amempongeza kijana huyo kwa kuweka picha yake kwenye bajaji kutokana na upendo wa dhati alionao ambapo aliamua kuweka picha hiyo kwenye bajaji kama zawadi kwake suala lilomgusa Mkurugenzi huyo na kuamua kutoa zawadi ya bajaji. “Bajaji hiii itamsaidia kuongeza kipato chake ,Namshukuru sana alifanya hivyo kwa mapenzi ya dhati kwangu kwani nimetoa hamasa kwa vijana wengi wa kitanzania kufanya kazi kwa bidi na kutimiza ndoto zao huku wakiendelea kusaidia jamii inayowazunguka” Anaeleza Mulokozi Mkurugenzi huyo wa Mati ametoa wito kwa madereva wa bajaji kutangaza bidhaa zinazozalishwa na kiwanda chake ikiwemo Tanzanite Royal Gin,Strong Dry G...

AJALI YAUA MTALII WA KICHINA SERENGETI ,6 WAJERUHIWA

Picha
Mtaalii mmoja mwenye asili ya China amefariki dunia na wengine sita wamejeruhiwa baada ya gari la Watalii lenye namba za usajili T603 DCL mali ya Kampuni ya Yonda Africa walilokuwa wanalitumia, kupata ajali likiwa njiani kurudi hotelini kilomita moja kutoka Lobo Wildlife Lodge katika Hifadhi ya Taifa Serengeti. Taarifa iliyotolewa usiku huu na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) imesema “Majira ya saa 10 jioni July 28,2024 gari la Watalii lenye namba za usajili T603 DCL mali ya Kampuni ya Yonda Africa lilipata ajali likiwa njiani kurudi hotelini kilomita moja kutoka Lobo Wildlife Lodge katika Hifadhi ya Taifa Serengeti” Gari hiyo ilikuwa na Watalii saba wenye asili ya China na Dereva Raia wa Tanzania, Mgeni mmoja alifariki dunia na wengine 6 walipata majeraha, mwili wa Marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Mugumu na majeruhi sita wanaendelea kupata matibabu katika Hospitali hiyo” Uchunguzi unaendelea kwa kushirikiana na Mamlaka nyingine ili kubaini chanzo cha ajali hiyo”

KANISA LA KIBOKO YA WACHAWI LAFUNGWA LINADHALILISHA KWA MAHUBIRI YA OVYO

Picha
SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeagiza kufungwa Kanisa la Christian Life Church linaloongozwa na Mchungaji Domique Kashoix Dibwe maarufu Kiboko ya Wachawi, lililopo Buza Kwa Lulenge, Temeke - Dar es Salaam baada ya kanisa hilo kwenda kinyume cha taratibu za usajili. Barua ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Ofisi ya Msajili wa Jumuiya za Kiraia ya Julai 25, 2024 imewaelekeza Mwenyekiti wa Kanisa la Christian Life Church na Mchungaji Dominique Kashoix Dibwe kufunga tawi la Kanisa hilo linaloendeshwa na mchungaji huyo.  Miongoni mwa sababu zilizotajwa za kufungwa kwake ni kutoa mafundisho yenye kuleta taharuki katika jamii na mahubiri ambayo ni kinyume na maadili, mila, desturi na utamaduni wa Kitanzania.  Madai mengine ni kutoa mahubiri yanayodhalilisha watu madhabahuni, kutoa mahubiri chonganishi na kuhamasisha waumini wa kanisa lake kuua watu kwa dhana au tuhuma za uchawi au ushirikina. Baada ya kusambaa taarifa kwenye mitandao ya kijamii kwamba Serikali...

RC MAKONDA AKABIDHI MILIONI 38 KWA WASHINDI WA SAMIA MOTOCROSS CHAMPIONSHIP

Picha
Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda amekabidhi jumla ya fedha taslimu shilingi Milioni 38 za Kitanzania kwa washindi wa vipengele mbalimbali vya mashindano ya pikipiki ya Samia Motocross Championship. Kelvin Gabriel ndiye aliyetangazwa kama mshindi wa jumla kwenye mashindano hayo akiondoka na fedha taslimu shilingi Milioni kumi za Kitanzania ambapo Mkuu wa Mkoa Mhe. Makonda ameahidi pia kuwashika mkono kwenye kushiriki michuano ya kikanda na Kimataifa. Msisimko mkubwa pia umekuwa kwa ndugu pacha Yannick Allad na Manuel Allard ambao wameibuka mshindi wa kwanza na wa pili kwenye kundi la Inter Midietly, wakikiri wazi kuwa baba yao mzazi amekuwa msaada mkubwa na mwalimu wao katika kukimbiza pikipiki.

WAMAREKANI WAMCHOKA RAIS BIDEN,WAMTAKA AACHIE NGAZI,YEYE ANG'ANG'ANA KUGOMBEA ANA MIAKA 81

Picha
  Home HABARI ZA KIMATAIFA WAMAREKANI WAMCHOKA RAIS BIDEN,WAMTAKA AACHIE NGAZI,YEYE ANG'ANG'ANA KUGOMBEA ANA MIAKA 81 Rais wa Marekani Joe Biden Jumatano ameapa kuendelea kuwania muhula wa pili, akipuuza hisia zinazozidi kuongezeka kwamba kushindwa kufanya vizuri katika mdahalo wa kwanza, kutasababisha ajiondowe kwenye kampeni kuelekea uchaguzi wa tarehe 5 Novemba. “Ninagombea. Mimi ni kiongozi wa chama cha Democratic. Hakuna anayenishurutisha kujiuzulu,” Biden aliwambia washauri wake, kulingana na afisa wa kampeni yake. Biden na Makamu Rais Kamala Harris walijitokeza gafla katika mkutano wa kamati kuu ya chama cha Democratic kwa njia ya mtandao, wakiutumia kama fursa ya mazungumzo ya kina na kusisitiza umuhimu wa uchaguzi wa 2024. Biden alisema atasimama tena imara baada ya kuanguka kutokana na kushindwa kufanya vizuri katika mdahalo wa wiki iliyopita. Uhakikisho wa Biden kwamba atabaki kwenye kinyang’anyiro unajiri huku baadhi ya Wademocrats wakiwa wameanza kuhoji hadharani i...

MENEJA TRA MBARONI KWA KUSAFIRISHA MENO YA TEMBO,AKUTWA PIA NA NAMBA KIBAO ZA MAGARI ,APAMBANA KUZIMA TUKIO KINYEMELA,TIZANA PICHA ZA TUKIO

Picha
  Jeshi la Polisi Wilaya ya Kibondo Mkoa wa Kigoma linamshikilia Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Wilayani humo Irving Mutegeki kwa tuhuma za kukutwa na meno ya Tembo. Mutegeki Bagasheki amekamatwa na nyara hizo za Serikali Wilaya ya Kibondo Julai 2,2024 akiwa kwenye gari binafsi majira ya usiku na anaendelea kushikiliwa na jeshi la polisi kwa ajili ya mahojiano zaidi. Meneja huyo wa TRA anadaiwa amekuwa akifanya biashara ya meno ya Tembo kutoka Wilaya ya Kibondo na Kakonko kwenda mikoa mbalimbali nchini na nje ya nchi ikiwemo Burundi. Hata hivyo kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na taarifa za mauaji ya Tembo katika misitu na hifadhi zilizopo katika wilaya ya Kibondo na Kakonko. Taarifa kutoka Wilayani humo inaonyesha kuwa kuna jitihada za kuficha suala hilo kwa kutengenezwa mazingira ya rushwa ili kulimaliza jambo hilo ambalo ni uhujumu uchumi.