KIVUTIO CHA UTALII UHAMAJI WA NYUMBU NI ZAO LA UTAFITI
Ikiwa tarehe 27 Septemba kila mwaka Mataifa mbalimbali huadhimisha Siku ya Utalii Duniani, Tafiti za Wanyamapori zimeendelea kuchangia kukua kwa Utalii ambapo ugunduzi wa Kivutio kikubwa cha Utalii cha tukio la kiasili la Uhamaji wa Nyumbu (The Great Migration) ni zao la Utafiti. Mtafiti wa Nyumbu kutoka Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) Dkt. Emmanuel Masenga amesema tafiti za wanyamapori zimechochea kuimarika kwa uhifadhi na kukuza utalii ambapo kivutio cha kuhama kwa nyumbu ndani ya hifadhi ya Taifa Serengeti ni zao la tafiti za miaka ya 1950 "Mtafiti Prf. Bernard Grzimek ndie mgunduzi wa kivutio hiki" amebainisha Dkt. Masenga. Aidha, Dkt. Masenga amesema mbali na ugunduzi wa kivutio cha kuhama kwa Nyumbu, TAWIRI imeendelea kufanya tafiti mbalimbali zinazolenga kuimarisha uhifadhi wa nyumbu ambapo zimesaidia kubaini na kuhifadhi maeneo wanayozaliana kwenye mbuga za nyasi fupi kusini mwa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Pori la Akiba M...