NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA ELIMU ATOA RAHI UFANISI KATIKA UTOAJI WA ELIMU BORA
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Charles Mahera amesema katika zama hizi za maendeleo ya Sayansi na Teknolojia, Uhitaji wa matumizi ya TEHAMA katika ufundishaji na ujifunzaji ni hitaji muhimu na lisiloepukika kwa ajili ya kurahisisha ufanisi katika utoaji Elimu bora. Ameyasema hayo leo Disemba 18, 2024, akimwakilisha katibu Mkuu Prof Carolyne Nombo Katika Ufunguzi wa Mafunzo ya Matumizi Bora na salama ya vifaa vya TEHAMA na stadi za kidigitali kwa walimu wa Awali na Msingi Dkt. Mahera amesema Serikali kupitia programu ya BOOST Serikali ina dhamira ya kusambaza vifaa vya TEHAMA katika Vituo vya Walimu au Shule teule zipatazo 800 na kwa awamu ya Kwanza, vifaa hivyo vya TEHAMA vimeshasambazwa katika Vituo 200 vikiwemo Vituo vya Walimu 57 na Shule Teule 143 nchini "Kwa mwaka huu Serikali kupitia Programu ya BOOST itanunua na kuweka vifaa vya TEHAMA katika Vituo vya Walimu na Shule Teule 600 zilizobaki ili kukamilisha Vituo vya Walimu/Shule Teule 800...