Machapisho

KRFA yachora ramani mpya ya soka Kilimanjaro, yabana mashindano holela

Picha
KRFA imepitisha maazimio ya kuimarisha maendeleo ya soka Kilimanjaro, yakiwemo kudhibiti mashindano holela (ndondo), kuzuia udanganyifu wa umri, kuibua vipaji na kuongeza waamuzi, katika mkutano mkuu wa kawaida uliofanyika Moshi. Moshi.Chama cha Soka Mkoa wa Kilimanjaro (KRFA) kimekuja na ramani mpya ya maendeleo ya soka mkoani humo baada ya kupitisha maazimio kadhaa yatakayobana mashindano holela, kuibua vipaji vya vijana na kuongeza idadi ya waamuzi. Maazimio hayo yamepitishwa katika mkutano mkuu wa kawaida wa chama hicho uliofanyika Moshi, huku viongozi wakisisitiza kuwa muda wa kuendesha soka bila utaratibu umefikia mwisho. Maazimio hayo yamepitishwa katika mkutano mkuu wa kawaida wa chama hicho uliofanyika katika ukumbi wa mkutano wa Chuo Kikuu Cha Ushirika Moshi, huku viongozi wakisisitiza kuwa muda wa kuendesha soka bila utaratibu umefikia mwisho. Akizungumza leo Juni 1,2026 baada ya kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa mkutano wa Chuo Kikuu Cha Ushirika Moshi,Katibu wa ...

TAARIFA ZA TEKNOLOJIA YA MIKANDA YA VISUKUMA MAWIMBI KUKUZA UTALII

Picha
Afisa Mhifadhi Mkuu kutoka TANAPA, Davis Mushi amesema zoezi la kuwafunga tembo teknolojia ya mikanda ya visukuma mawimbi mbali na kudhibiti makundi ya tembo yanayoleta changamoto kwa wananchi, taarifa za teknolojia hiyo zitachochea utalii na uhifadhi wa tembo kwa huonesha mienendo ya tembo katika misimu mbalimbali ya mwaka. Mtafiti na daktari wa wanyamappri kutoka TAWIRI Dkt.Mikidadi Mtalika amesema zoezi hilo limelenga kufuatilia zaidi ya tembo mia moja katika Wilaya za Kilombero na Morogoro Vijijini ambapo hadi tarehe 12 Mei, 2026 tembo viongozi wa makundi manne (4) yenye zaidi ya tembo 40 wamefungwa mikanda ya visukuma mawimbi na zoezi linaendelea. Wakati zoezi hilo likiendelea, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Six Rivers Afrika, Bw. Brandon Kempt, akiwa uwandani ametangaza neema kwa TANAPA na TAWIRI “Wanafanya kazi nzuri, sisi kama wadau wa kimataifa hatuna budi kuhamasisha dunia kuthamini urithi wa maliasili iliyopo Tanzania na kutuunga mkono kuziwezesha TANAPA na TAWIRI kutek...

*BALOZI KAGANDA ATEMBELEA OFISI ZA TPA NCHINI ZIMBABWE*

Picha
Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Kamishna wa Polisi (CP) Suzan Kaganda, ametembelea ofisi za Mamlaka ya Bandari ya Tanzania (TPA) zilizopo mjini Harare na kufanya mazungumzo na Mwakilishi wa TPA nchini humo, Bi. Kulthum Boma kuhusu namna ya kuimarisha huduma na kuongeza ufanisi katika usafirishaji wa mizigo kupitia bandari za Tanzania. Ziara ya Mheshimiwa Balozi Kaganda ni sehemu ya utekelezaji wa Sera ya Diplomasia ya Uchumi, ikiwa na lengo la kutambua na kuendeleza mchango wa TPA katika usafirishaji wa mizigo kutoka bandari za Tanzania kwenda nchi za Kusini mwa Afrika, ikiwemo Zimbabwe. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Bi. Kulthum Boma alieleza kuwa ofisi hiyo, yenye jukumu la masoko na huduma kwa wateja, imekuwa na mchango chanya katika kuongeza shehena ya mizigo inayoingia Zimbabwe kupitia bandari za Tanzania tangu kufunguliwa kwake rasmi mwaka 2023. Kwa upande wake, Mheshimiwa Balozi Kaganda amepongeza mafanikio hayo na kusisitiza umuhimu wa ushirikiano wa karibu kati ya ofisi...

KAMANDA MASIJA ATOA WITO DHIDI YA UHALIFU WA KIMTANDAO

Picha
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Shadrack Masija, ametoa wito kwa wananchi kuwa waangalifu wanapotumia mitandao ya mawasiliano na majukwaa ya kidijitali ili kujiepusha na vitendo vya uhalifu wa kimtandao vinavyoendelea kujitokeza katika jamii. Kamanda Masija ametoa wito huo Machi 13, 2026 wakati akishiriki futari (iftar) iliyoandaliwa na mtandao wa simu wa Yas katika Ukumbi wa Country Hotel uliopo Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa, hafla iliyowakutanisha wadau mbalimbali wa mawasiliano na wananchi. Akizungumza katika hafla hiyo, SACP Masija amesema kumekuwa na ongezeko la matukio ya uhalifu wa kimtandao ikiwemo utapeli kupitia simu na mitandao ya kijamii, ambapo baadhi ya watu hutumia teknolojia vibaya kwa lengo la kujipatia fedha au taarifa za wengine kwa njia zisizo halali. Kutokana na hali hiyo, amewahimiza wananchi kuwa makini wanapotumia simu na mitandao ya kijamii kwa kuepuka kutoa taarifa zao binafsi kwa watu wasiofahamika pamoja n...

BARAZA LA ARDHI LAFUTA KESI YA ARDHI KUTOKANA NA DOSARI ZA KISHERIA

Picha
Katika maombi hayo namba 83/2025 yalifunguliwa na Chemli Mallya dhidi ya Anna Mallya (ambaye ni shemeji yake),mgogoro unaotajwa kuwepo kwa zaidi ya miaka 10 tangu mume wa Anna ambaye ni kaka wa Chemli, Mathias Mallya,aliyefariki mwaka 2010 Moshi.Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya ya Moshi limelifuta shauri la ardhi linalowahusisha wanaukoo wa Mallya baada ya kubaini kuwa mleta maombi alikiuka amri ya awali ya marekebisho ya hati ya maombi. Uamuzi huo umetolewa Februari 24,2026 na Mwenyekiti wa Baraza hilo,Hussen Lukeha, baada ya kukubaliana na pingamizi la awali lililowasilishwa na mjibu maombi. Shauri hilo la maombi namba 83/2025 lilifunguliwa na Chemli Mallya ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Sisamaro, Kata ya Kibosho Okaoni,Wilaya ya Moshi Mkoa wa Kilimanjaro,mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miaka 10. Mjibu maombi katika shauri hilo ni Anna Midimito, mjane wa marehemu Mathias Mallya aliyefariki mwaka 2010, ambaye alikuwa mdogo wa mleta maombi,Chemli Mallya. Akitoa uamuzi huo Mwenyekiti hu...

ASKARI KUTOKA TANZANIA WAVISHWA NISHANI KUTAMBUA MCHANGO WA KULINDA AMANI SUDANI KUSINI..

Picha
Maafisa,na askari wa vyeo mbalimbali kutoka Jeshi la Polisi Nchini Tanzania ambao nikundi lilomaliza muda wake wa kuhudum kulinda amani nchini Sudan kusini wamehitimisha kwa Paredi maalum ambayo ili ambatana na kuwavisha nishani( Medall Pin) maafisa na askari hao ikiwatambua kwa kazi nzuri ya kudumisha amani. Tanzania ni miongoni mwa nchi bora zinazochangia askari wake katika Operesheni za kulinda amani za Umoja wa Mataifa. Aidha Miongoni mwa maafisa hao wamebainisha kuwa licha ya kuwa mazingira magumu ya iliwapa moyo kuendelea kulinda amani na kutoa elimu kwa makundi mengi zaidi. Sambamba na hilo wameendelea kuwashukuru maafisa wengine wa majeshi kwa namna walivyoshirikiana kudumisha amani katika misheni ya kulinda amani nchini Sudan Kusini Mwisho wamewaomba wananchi wa Sudan kusini kuendelea kutunza na kulinda amani ya nchini hiyo

ZARA TOURS YANG'ARA TENA KWENYE TUZO ZA SERENGETI, NA KUPANUA MFUMO WAKE WA HESHIMA ZA KIMATAIFA

Picha
Kampuni ya utalii ya Zara Tours ya mjini Moshi kwa mara nyingine imethibitisha uongozi wake katika sekta ya utalii nchini Tanzania baada ya kujinyakulia tuzo nyingine ya heshima kwenye tuzo za Serengeti, na kuendeleza msururu wa heshima ambao kampuni hiyo imekuwa ikijipatia karibu kila mwaka.  Tuzo hiyo ni miongoni mwa tuzo 51 zilizotolewa wakati wa hafla ya utoaji wa tuzo za Serengeti iliyofanyika usiku wa kuamkia jana kwenye hoteli ya Mount Meru jijini Arusha, hafla iliyowakutanisha wadau wakuu wa utalii kutoka Tanzania na nje ya nchi.   Naye Mgeni Rasmi Waziri wa Fedha Dkt.Mwigulu Nchemba ameipongeza sekta ya utalii kwa mchango wake mkubwa katika kukuza uchumi wa taifa, kutengeneza fursa za ajira na kuitangaza Tanzania duniani. Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo, Mkurugenzi wa Zara Tours, Bi. Zainabu Ansell alisema mafanikio hayo yanadhihirisha uchapakazi, ari ya pamoja na ushirikiano wa karibu kati ya serikali na wadau wa sekta binafsi hususan katika ulinzi na...