BARAZA LA ARDHI LAFUTA KESI YA ARDHI KUTOKANA NA DOSARI ZA KISHERIA
Katika maombi hayo namba 83/2025 yalifunguliwa na Chemli Mallya dhidi ya Anna Mallya (ambaye ni shemeji yake),mgogoro unaotajwa kuwepo kwa zaidi ya miaka 10 tangu mume wa Anna ambaye ni kaka wa Chemli, Mathias Mallya,aliyefariki mwaka 2010 Moshi.Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya ya Moshi limelifuta shauri la ardhi linalowahusisha wanaukoo wa Mallya baada ya kubaini kuwa mleta maombi alikiuka amri ya awali ya marekebisho ya hati ya maombi. Uamuzi huo umetolewa Februari 24,2026 na Mwenyekiti wa Baraza hilo,Hussen Lukeha, baada ya kukubaliana na pingamizi la awali lililowasilishwa na mjibu maombi. Shauri hilo la maombi namba 83/2025 lilifunguliwa na Chemli Mallya ambaye ni mkazi wa Kijiji cha Sisamaro, Kata ya Kibosho Okaoni,Wilaya ya Moshi Mkoa wa Kilimanjaro,mgogoro uliodumu kwa zaidi ya miaka 10. Mjibu maombi katika shauri hilo ni Anna Midimito, mjane wa marehemu Mathias Mallya aliyefariki mwaka 2010, ambaye alikuwa mdogo wa mleta maombi,Chemli Mallya. Akitoa uamuzi huo Mwenyekiti hu...