Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2025

TAMATI YA MAFUNZO YA SIKU TANO YA KUWAJENGEA UWEZO ASASI ZA KIRAIA ZINAZOPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA MIKOA YA KANDA YA KASKAZINI

Picha
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Kanda ya Kaskazini kwa kushirikiana na Taasisi ya Colombo Plan Drug Advisory Programme (CP-DAP) tarehe 28.03.2025 imehitimisha rasmi mafunzo maalum ya kuwajengea uwezo wawakililshi kutoka Asasi 25 za Kiraia zinalizopo Mikoa ya Kanda ya Kaskazini ambazo zinapambana na dawa za kulevya yaliyofanyika katika Ukimbi wa Amani Center uliopo Kaloleni jijini Arusha. Mafunzo hayo ya siku tano yalihusu Mtaala wa Kimataifa wa Utoaji Elimu Kinga Sahihi Dhidi ya Tatizo la Dawa za Kulevya (Universal Prevention Curriculum-UPC). Mafunzo hayo yalifanyika kwa muda wa siku tano mfululizo kuanzia tarehe 24.03.2025 ambapo Mgeni rasmi katika ufunguzi wa mafunzo hayo alikuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Arusha Mhe. Joseph Modest Mkude. Mgeni rasmi wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Machi 24, 2025 alikuwa Joseph Modest Mkude Mkuu wa Wilaya Arusha na Machi 28, 2025 yalifungwa rasmi na Katibu Msaidizi Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Kaskazin...

VIJANA ZAIDI YA 1, 000 WAJITOKEZA KWENYE USAHILI WA UFADHILI WA MASOMO NCHINI INDIA

Picha
Mapema leo Machi 26, 2025 vijana zaidi ya 1000 wa Mkoa wa Arusha wamejitokeza kwa katika ofisi za mkoa kwa ajili ya usahili wa kuwania nafasi za ufadhili wa masomo nchini India kufuatia tangazo la Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Paul Christian Makonda, aliyesema kuwa serikali ya India imetoa ufadhili wa masomo kwa vijana 1,000 wa Arusha. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa usahili huo, Mhe. Makonda amebainisha kuwa ufadhili huo utahusisha programu na fani zaidi ya 250, ufadhili huo ukisimamiwa na Serikali ya India kupitia kwa Balozi wake nchini Tanzania, Mhe. Bishwadip Dey. Mhe. Makonda ameeleza kuwa fursa hiyo imetokana na juhudi kubwa alizozifanya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuimarisha uhusiano na mzuri na Mataifa Mengine ambazo zimepelekea nchi kama India kutoa fursa hizo kwa vijana wa Kitanzania. "Hii ni fursa adhimu kwa vijana wa Arusha kupata elimu bora nje ya nchi, hususan nchini India, ambayo inajulikana kwa ubora wa elimu yake katik...

JK AWASILISHA UJUMBE MAALUMU KWA RAIS WA SENEGAL KUTOKA KWA RAIS SAMIA

Picha
Mhe. Rais Mstaafu  Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amewasilisha  ujumbe maalumu kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwenda kwa Rais wa Jamhuri ya Senegal, Mhe. Bassirou Diomaye Faye jijini Dakar. Katika mazungumzo  yao ya kirafiki,  Rais Mstaafu alieleza dhamira ya dhati ya Rais Samia na Serikali anayoiongoza ya kuendeleza na kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia, kiuchumi na kijamii kati ya Tanzania na Senegal. Pamoja na masuala ya ushirikiano wa kiserikali, Rais Mstaafu pia alisisitiza umuhimu wa kukuza uhusiano baina ya wananchi wa mataifa haya mawili kupitia sekta za elimu, biashara, utalii, na maendeleo ya vijana na wanawake. Ziara hii ni sehemu ya juhudi endelevu za Tanzania kuimarisha uhusiano wa kimataifa na mataifa ya Afrika Magharibi, huku ikiweka msisitizo kwa diplomasia ya uchumi na ushirikiano wa watu kwa watu.

UJUMBE KUTOKA ZANZIBAR WAJIFUNZA MBINU MPYA POLISI UTALII ARUSHA.

Picha
Ujumbe kutoka Idara ya Utalii na mambo ya kale Zanzibar katika kuhakikisha wanaendelea kutoa huduma bora kwa wageni na watalii wanaofika nchini kwa ajili ya mapumziko na utalii wamefika Jijini Arusha kwa lengo la kujifunza katika kituo cha Polisi utalii na Diplomasia namna wanavyofanya kazi na kutoa huduma kwa wageni hapa nchini. Akiongea mara baada ya mafunzo hayo yaliyofanyika katika kituo cha Utalii na Diplomasia Arusha Mkurungenzi wa Idara ya Utalii na Mambo ya kale Zanzibar Daktari Abdallah Mohamed amesema kuwa moja ya mtaji mkubwa katika biashara ya utalii ni ulinzi na usalama wa eneo husika ambapo amebainisha kuwa mafunzo hayo yamewapa dira na namna ya Kwenda serikali ya mapinduzi Zanzibar kuboresha utendaji kazi wao. Dkt Mohamed ameongeza kuwa wamekuja Arusha kwa sababu ya uwepo wa kituo hicho cha mfano katika kutoa huduma kwa watalii na wanadiplomasia wanaofika nchini kwa shughuli mbalimbali ambapo amesisitiza kuwa mafunzo hayo yamewajenga na kuongeza mbinu katika utendaji bor...

INEC YAONGEZA SIKU UBORESHAJI DAFTARI LA WAPIGA KURA DAR

Picha
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza kuongeza siku mbili zaidi za zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Mkoani Dar es Salaam ambapo sasa zoezi hilo litamalizika Machi 25, 2025. Hatua hiyo imetangazwa na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele leo Machi 23, 2025 kufuatia mwitikio mkubwa wa wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam ambao kujitokeza kwa wingi katika zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ulioanza Machi 17 na uliotarajiwa kumalizika leo Machi 23 mwaka huu. “Hivyo basi, napenda kuwatangazia wananchi wote wa mkoa wa Dar es Salaam kuwa, Tume imeongeza siku mbili za uboreshaji wa Daftari kwa tarehe 24 na 25 Machi, 2025 na zoezi litakamilika tarehe 25 Machi, 2025 saa 12:00 jioni,” amesema Jaji Mwambegele. Aidha, Jaji Mwambegele amefafanua kuwa baada ya siku hizo mbili Tume haitaongeza muda zaidi. Amesema wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wamekuwa na mwitikio mkubwa wa kujitokeza kujiandikisha na kubores...

DCEA YATOA MAFUNZO MAALUM KWA WATOTO WA MTAANI JIJINI ARUSHA

Picha
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Kanda ya Kaskazini kwa kushirikiana na Kituo cha Kulea Watoto wa Mtaani cha Amani Center tarehe 18.03.2025 imetoa mafunzo maalum juu ya mbinu za kujiepusha na tatizo la dawa za kulevya kwa watoto wa mtaani 9 waliopo katika kituo cha Amani Center kilichopo Ngarenaro jijini Arusha.  Watoto hao wa mtaani ambao wapo katika hatari kubwa ya kuingia katika matumizi ya dawa za kulevya walifundishwa mbinu mbalimbali za kujizuia na vishawishi vinavyoweza kuwapelekea kutumia dawa hizo.  *Pia walihimizwa kushirikiana na Mamlaka kutoa taarifa za wahalifu wa dawa za kulevya kupitia namba ya simu ya bure ya 119 ili kuhakikisha watu wanauza dawa mitaani wanaweza kudhibitiwa kwa mujibu wa sheria*

MSOMERA WAFIKIWA NA ELIMU YA UNENEPESHAJI MIFUGO KUPATA MAZAO BORA YA NYAMA.

Picha
Katika kuhakikisha bodi ya Nyama Tanzania (TMB) inazifikia jamii hususani zile za kifugaji imeendelea kutoa elimu ya ufugaji bora katika kunenepesha mifugo ili kupata  mazao bora ya nyama  Mkoani Tanga katika Wilaya ya Handen Kijiji cha Msomera. Akitoa elimu afisa Mifugo Festo Nzalallila amewaomba wafugaji kufuata taratibu za ufugaji na malisho sahihi ya mifugo yao ili kupata mazao mazuri ya nyama ambapo amebainisha kuwa kwa kufanya hivyo kutaongeza soko la biashara hiyo ya mazoa ya nyama ndani na nje ya nchi. Aidha afisa huyo wa mifugo amewambia wananchi wa msomera kuwa eneo hilo kwa ufugaji na malisho ni zuri hivyo anaimani mazao ya nyama yatakuwa bora na kuwafutia walaji wa nyama kutoka Msomera. Vilevile amewasisitiza wafugaji hao kuwa ni vyema wakafanya ufugaji wa kisasa ambao matokeo yake ni mazuri kibiashara husu akigusia suala la unenepeshaji wa mifugo ili kupata mazao bora ya nyama.

RAIS MSTAAFU Dkt.JAKAYA KIKWETE AKIWA KATIKA MAZUNGUMZO NA BW.YOHEI, MWENYEKITI WA TAASISI YA NIPPO, NA MAOFISA WAKE WAANDAMIZI JIJINI TOKYO.

Picha
Rais mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa  Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Elimu la Kimataifa (GPE), yupo Tokyo nchini Japan kwa ziara maalum yenye lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya GPE na serikali ya Japan katika kutatua changamoto za elimu ya msingi katika nchi zinazoendelea.   Katika siku yake ya kwanza Tokyo, Dkt. Kikwete amefanya mazungumzo na Waziri wa Fedha wa Japan, Mhe. Shin-ichi Yokohama, pamoja na Naibu wake, Mhe. Atsushi Mimura. Mazungumzo hayo yalijikita katika ushirikiano wa kifedha ili kusaidia miradi ya elimu inayosimamiwa na GPE, ikiwemo upatikanaji wa rasilimali kwa ajili ya kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto wa nchi zinazoendelea.   Baada ya mazungumzo hayo, Rais Mstaafu Kikwete alikutana na Bw. Akihiko Tanaka, Rais wa Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Japan (JICA). Shirika hili limekuwa na mchango mkubwa katika miradi ya maendeleo barani Afrika, na mazungumzo yalihusu namna JICA inaweza kusaidia jitihada za GPE katika kukuza...

DCEA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE KIMATAIFA JIJINI ARUSHA

Picha
  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Kanda ya Kaskazini tarehe 08.03.2025 inaungana na Watanzania, Taasisi za umma na Sekta binafsi katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Kimataifa kwa kutoa elimu kwa jamii juu ya madhara ya tatizo la dawa za kulevya katika viwanja vya TBA vilivyopo Kaloleni jijini Arusha.  Mgeni rasmi alikuwa ni Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye alihutubia umma katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid. Kaulimbiu ya Maadhimisho hayo ni; *Wanawake na Wasichana 2025:* *_Tuimarishe Haki, Usawa na Uwezeshaji_*. Wananchi waliofika katika banda la Mamlaka walipata fursa ya kuona aina za sampuli mbalimbali za dawa za kulevya lakini pia kuona bidhaa mbalimbali zilizotengenezwa na waraibu waliopata nafuu kamavile sabuni na mikate.   *_Wananchi waliofika katika banda la Mamlaka waliombwa kushirikiana na Mamlaka kwa kutoa taarifa za wahalifu wa dawa za kulevya kupitia Kituo cha Miito ya Simu cha Mamlaka kwa kupiga simu ya bur...

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KATIKA KONGAMANO LA WANAWAKE JIJINI ARUSHA

Picha
Imeelezwa kuwa zaidi ya 60% ya wafanyakazi wa moja kwa moja kwenye sekta ya utalii ni wanawake licha ya kukabiliwa na changamoto lukuki kwenye sekta hiyo inayochangia zaidi ya 17% ya pato la Taifa. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano la wanawake jijini Arusha kuelekea maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga Taifa Dkt. Stergomena Tax amesema watahakikisha wanawake wananufaika zaidi na fursa zilizopo kwenye sekta hiyo. Kwa upande wake naibu waziri wa maendeleo ya jamii jinsia wanawakena makundi maalum Mwananidi Ali Khamis anasema Rais Samia ameshafungua milango ya watalii hivyo wanawake wa Arusha na mikoa mingine wachangamkie fursa hiyo. Dkt. Bakari George, Mkuu wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru (TICD) ambacho kina kituo cha utafiti na uhifadhi wa machapisho ya wanawake anasema Rais Samia hajahamasisha wanawake tu kwenye maswala ya uongozi bali hata wanaume. Kongamano hilo la wanawake limebebwa na kaulimbiu isemayo ushiriki wa wanawake ka...